Umoja wa Mataifa wajadili amani kwenye ukanda wa maziwa makuu
Kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani, kumefanyika mkutano wa sita wa kikanda kuhusu mchakato wa amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC na ukanda wa maziwa makuu, ukiangazia makubaliano ya amani, ulinzi na usalama yaliyopitishwa mwezi Februari mwaka 2013 huko Addis Ababa, Ethiopia.
Akizungumza kwenye mkutano huo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amegusia umuhimu wa amani na usalama akigusia suala la uchaguzi unaokaribia kwenye baadhi ya nchi za ukanda huo.
(Sauti ya Ban)
“Baadhi ya nchi kwenye ukanda wa maziwa makuu zinatarajia kufanya uchaguzi muhimu. Nasihi serikali na viongozi kuwajibika kwa ajili ya wananchi kwa kuheshimu katiba zao za kitaifa pamoja na mkataba wa Afrika kuhusu demokrasia, uchaguzi na utawala. Uchaguzi ni hatua muhimu kwenye demokrasia changa. Tunapaswa kuhakikisha nchi za ukanda huo zinatoka na nguvu na ushirikiano zaidi kutokana na utaratibu huo.”
(Sauti ya Belliard)
Aidha amemulika hali ya vurugu nchini Burundi akitoa wito..
(Sauti ya Belliard)