Sera madhubuti zahitajika kukabiliana na uhalifu kwa wanawake kupitia intaneti: Phumzile
Licha ya Teknlojia ya Habari na Mawasiliano kuchangia pakubwa katika maendeleo duniani, wanawake bado wanakumbwa na changamoto chungu nzima zinatokana na mlipuko wa mtandao wa Intaneti.
Hii ni kwe mujibu wa repoti iitwayo vita dhidi ya wanawake na wasichana, wito kwa dunia kuchua hatua iliyoandaliwa na kikundi kazi cha Umoja wa Mataifa kuhusu Maendeleo ya dijitali na jinsia
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa repoti ya jopo hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake, UN Women, Phumzile Mlambo-Ngcuka, amesema uhalifu dhidi ya wanawake kwenye mtandao wa intaneti ni sawa na dhuluma zinazotendeka kwingineko na akataka kuwepo katika kukabiliana na ukatili huo.
(SAUTI NGCUKA)