Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Maonyesho ya Milan Expo yalenga kutokomeza njaa

Maonyesho ya Milan Expo yalenga kutokomeza njaa

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Mpango wa Chakula, WFP, Ertharin Cousin, alimshukuru nyota wa bendi ya muziki ya U2 na mwanzilishi wa ONE, Bono, na Waziri Mkuu wa Italia, Matteo Renzi kwa juhudi zao za kupaazia sauti watu maskini na wenye njaa duniani.

Bono na Bi Cousin walikutana Jumapili Agosti 6 kwenye hafla maalum iitwayo, “Inaanza nami” kwenye maonyesho ya Expo Milan 2015. Hafla hiyo ililenga kuchagiza watu katika jitihada za kutokomeza njaa na kuongeza uelewa wa haja ya rasilmali zaidi za kushughulikia mahitaji yanayoongezeka ya chakula kwa watu wanaokimbia migogoro. Kwa mengi zaidi, ungana na Joshua Mmali katika makala hii