Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

ILO na Japan zaleta nuru kwa vijana wa Garissa nchini Kenya

ILO na Japan zaleta nuru kwa vijana wa Garissa nchini Kenya

Nchini Kenya, suala la ukosefu wa ajira ni mwiba zaidi kwa vijana wa kike na kiume. Vijana walio na vyeti na shahada wanahaha kusaka ajira au kujiajiri ili kuboresha maisha yao. Hata hivyo nuru imeshuka huko Garissa nchini Kenya ambapo

Shirika la kazi duniani, ILO kwa ushirikiano na serikali ya Japani wameibuka na mradi wa kuwezesha vijana kujiajiri ambapo wanapatiwa stadi mbali mbali ikiwemo za ujenzi. Je nini kimefanyika? Ungana na Joseph Msami katika makala hii.