Tanzania kuadhimisha miaka 70 ya UM kwa kutunza mazingira
Katika kuadhimisha miaka 70 ya Umoja wa Mataifa Tanzania imesema itaadhimisha siku hiyo kwa matukio kadhaa ya kutunza mazingira ikiwamo upandaji miti ikiwa ni sehemu ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
Katika mahojiano na afisa habari wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania Stella Vuzo
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Celestine Mushy anafafanua .
(SAUTI BALOZI MUSHY)
Amesema tangu uwepo wa Umoja wa Mataifa Tanzania mwaka 1961, chombo hicho kimetoa mchango mkubwa katika ujenzi wa amani , na mendeleo katika sekta kama vile elimu na afya pamoja na kuondoa umasikini.