Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Watoa misaada ya kibinadamu wapewe kipaumbele: OCHA

Watoa misaada ya kibinadamu wapewe kipaumbele: OCHA

Tuwashemu na kuwapa kipaumbele watoa misaada kwani wanafanya kazi nyeti katika maeneo yenye majanga. Amesema mtaalamu mweza wa menejimenti ya mpango katika ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya kibinadamu OCHA, Sarah Oseombo.

Katika mahojiano na Joseph Msami wa idhaa hii kuhusu maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kibinadamu, Bi Osembo amesema inasikitisha kuona bara analotoka Afrika, linakabiliwa zaidi na majanga ya kibinadamu ambayo yanaweza kuepukika,  lakini akaenda mbali ziaid kuwa kwa kuwa yameshatokea usaidizi wa kibainadmau ni muhimu na haukwepeki.

Kwanza Bi Osembo anaanza kwa kueleza umuhimu wa siku ya kimataifa ya misaada ya kibinadamu.