Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jumuiya ya kimataifa ihakikishe wanafunzi wa UNRWA wanarejea shuleni: UNESCO

Jumuiya ya kimataifa ihakikishe wanafunzi wa UNRWA wanarejea shuleni: UNESCO

Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la elimu sayansi na utamaduni UNESCO Irina Bokova ameelezea kusikitishwa kwake kufuatia ukosefu wa fedha uliosababisha kufungwa kwa shule za shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa Palestina UNRWA.

Katika barua yake kwa Kamishna Mkuu wa UNRWA Mr Pierre Krahenbühl., Bi Bokova amesema kuwa kwa watoto 500,000,  vigori pamoja na vijana 7,000 ambao wamekuwa wakipata mafunzo katika vituo vya UNRWA, elimu ni msingi wa kujenga mustakhabali mwema wa maisha yao.

Amesema ni jukumu la jumuiya ya kimataifa kuhakikisha fursa za kusoma kwa wote ili kuhakikisha wanafunzi wa UNRWA wanarejea shuleni kwa wakati.