Ban alaani shambulio la bomu Pakistan
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataiaf Ban Ki-moon, amelaani vikali shambulio la bomu hii leo jimboni Punjab nchini Pakistan, lilosababaisha majeruhi na vifovya watu kadhaa ikiwamo waziri wa mambo ya ndani wa nchi hiyo Shuja Khanzada.Grace Kaneiya na taarifa kamili.
(Taarifa Grace)
Taarifa ya msemaji wa Katibu Mkuu inamnukuu Bwana Ban akisisistiza kuwa hakuna kitu cha kuhalalisha ugaidi na kuelezea matumaini yake kuwa watekelezaji wa matukio hayo watafikishwa katika vyombo vya sheria.
Katibu Mkuu ametuma salamu zake za rambirambi kwa familia ,waathiriwa na kuwatakia uponyaji wa haraka majeruhi pamoja na kuelezea masikitiko yake kwa watu na serikali ya Pakistan.