Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mchango wa nyota wa Barcelona kwa watoto

Mchango wa nyota wa Barcelona kwa watoto

Klabu ya Uhispania ya soka FC Barcelona imo katika ziara ya Amerika Kaskazini, kabla ya msimu mpya wa soka kuanza mnamo mwezi Agosti. Katika hafla moja iliyoandaliwa na Shirika la Kuhudumia Watoto, UNICEF na klabu hiyo ya FC Barcelona, kundi la wanafunzi kutoka mji wa Los Angeles jimboni California, walikutana na nyota wa Barcelona, Andrés Iniesta na Marc-André Ter Stegen kujadili mchango muhimu wa michezo katika maisha ya watoto na maendeleo yao kote duniani.

Kufahamu zaidi yaliyotokea, ungana na Grace Kaneiya katika Makala hii.