Kay alaani shambulio la kigaidi mjini Mogadishu
Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa Somalia Nicholas Kay amelaani shambulio la Kigaidi linalodaiwa kutekelezwa na Al Shabaab lililosababisha watu kadhaa kuuwawa na wengine kujeruhiwa nchini humo. Taarifa zaidi na John Kibego.
(Taarifa ya Kibego)
Akilaani vikalio shambulio hilo lilkitokea kwenye Hoteli ya Jazeera katika mji mkuu wa Somalai Mogadishu, Bwana Nicholas Kay amesema, wauaji hao wanapaswa kuwajibishwa kisheria haraka iwezekanavyo.
Ametuma salamu za rambiramabi kwa serikali ya Somalia, familia na marafiki za waliouwauwa wakiwemo Mbunge Abdulahi Hussein Mohamud na Sai'd Ali Saleh, maafisa wa serikali waliouwauwa kwa kupigwa risasi.
Bwana Kay amewapongeza wanausalama wa Somalia kwa kuitikia shambulio hilo na kusisitiza kuwa Umoja wa Mataifa na wadau wake watandelea na juhudi zao kutimiza ndoto ya Wasomali ya kupata utulivu katika siku za baadaye.