Afrika yajipanga kukuza biashara kimataifa : Mero
Mkutano wa siku mbili kuhusu msimamo wa bishara ya kimataifa barani Afrika umemalizika leo mjini Nairobi nchini Kenya ambapo wawakilishi kutoka nchi mbalimbali barani humo wanaandaa wanachotaka kifanyike ili kuwezesha biashara na maendeleo barani humo.
Miongonimwa wanaohudhuria ni balozi wa kudumu wa Tanzania katika ofisi ya Umoja wa mataifa mjini Geneva Modest Mero ambaye katika mahojiano maalum na idhaa hii anaeleza kile walichokubaliana kuelekea mkutano wa dunia wa shirika la kimataifa la bishara (WTO) utakaofanyika mwezi Desemba mjini Nairobi.
(SAUTI)
Amesema masuala mengine kama ya hakimiliki pia yanajadiliwa kwa maslahi ya bara hilo kibiashara.