Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mapigano yazuka kaskazini mwa Darfur: UNAMID

Mapigano yazuka kaskazini mwa Darfur: UNAMID

Ujumbe wa pamoja wa Muungano wa Afrika na Umoja wa Mataifa jimboni Darfur nchini Sudan UNAMID umeripoti taarifa za kukua kwa mapigano kaskazini mwa nchi kulikochochewa na wizi wa mifugo.

Kwa mujibu wa msemaji wa Katibu Mkuu wa UM Stéphane Dujarric, UNAMID imeyataka makabila katika mzozo huo ambayo ni Rizeigat na Habaniya kufanya majadiliano ili kutatua mzozo huo na pia.

(SAUTI DUJARRIC)

‘‘Kujizuia katika vitendo vyote vinavyoweza kusababisha kukua kwa mgogoro, vifo na ukosefu wa makazi.’’

Amewaambia waandishi wa habari kuwa UNAMID inafuatilia kwa karibu mgogoro huo na kutoa usaidizi katika juhudi za kuzuia kuendelea kwa mapigano.