Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vijana wasaidiwe kujenga mustakhabali wa dunia: Ban

Vijana wasaidiwe kujenga mustakhabali wa dunia: Ban

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ametaka  jumuiya ya kimataifa kusukuma usaidizi kwa vijana ili kuimarisha uwezo wao katika kusaidia mustakabali wa pamoja wa dunia. Taarifa kamili na Priscilla Lecomte.

 (TAARIFA YA PRISCIILA)

Katika ujumbe wake wa kuadhimisha siku ya kimataifa ya ujuzi kwa vijana inayoadhimishwa leo Julai 15 kwa mara ya kwanza, Bwana Ban amesema wakati kote duniani vijana wakiwa na fursa ya elimu kuliko siku za nyuma, bado vijana barubaru 75 milioni hawako shuleni hatua inayotishia upatikanaji wa ujuzi wanaohitaji.

Kwa upande wake mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu vijana  Ahmed Alhendawi ambaye yuko mjini Addis Ababa,  Ethiopia  kuhudhuria kongamano la tatu la  kimataifa kuhusu ufadhili kwa maendeleo  linalozungumzia uwekezaji kwa vijana  anasema

 (SAUTI AHMED)

‘‘Tutumie fursa hii kuu kufikiria uwekezaji mkubwa kwa kizazi hiki na kuwahusisha katika kufikiria sera zitakazo wawezesha kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya nchi yao.’’

 Akizungumzia  fursa za ajira kwa vijana Ridhiwani Kikiwete ambaye ni kijana mbunge kutoka nchini Tanzania ameiambia iidhaa hii.

 (SAUTI RIDHIWANI)