Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uganda yajitutumua katika kukuza elimu ya msingi

Uganda yajitutumua katika kukuza elimu ya msingi

Wakati malengo ya maendeleo ya milenia MDGS yakifikia ukomo mwezi Septemba mwaka huu, nchi kadhaa zimejitahidi kutimiza malengo hayo manane likiwemo lengo namba mbili la kukuza elimu ya msingi kwa wote ambapo nchini Uganda serikali kwa kushirikiana na wadau imepiga hatua.

Hatua hizo zimesaidia wanafunzi wengi kujiunga shuleni na hivyo kuanza safari ya kutimiza ndoto zao kama anavyosimulia John Kibego kutoka nchini humo.