Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Umoja wa Mataifa wakumbuka kusainiwa kwa Katiba yake

Umoja wa Mataifa wakumbuka kusainiwa kwa Katiba yake

Mnamo Ijumaa Juni 26, hafla mbili tofauti ziliafanyika kuadhimisha miaka 70 tangu kusainiwa kwa Katiba ya Umoja wa Mataifa, ambayo kwayo, Umoja huo ulianzishwa. Hafla moja ilifanyika mjini San Francisco, jimbo la California, ambako katiba hiyo ilisainiwa mnamo Juni 26, mwaka 1945. Hafla ya pili ilifanyika kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York. Katika Makala hii, Joshua Mmali anatumegea kidogo yaliyokuwemo katika matukio hayo.