Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Haki ya ardhi kwa wakazi wa Hoima waliokumbwa na miradi ya visima vya mafuta

Haki ya ardhi kwa wakazi wa Hoima waliokumbwa na miradi ya visima vya mafuta

Nchini Uganda, harakati za kuanza kuchimba mafuta zimekuwa ni mwiba kwa baadhi ya wananchi ambao wanapaswa kupisha maeneo hayo kwa ajili ya miradi husika. Mathalani katika wilaya ya Hoima, mradi wa ujenzi wa kiwanda cha kusafisha mafuta tayari umesabaisha kuhama kwa asilimia 90 ya wakazi waliokuwa wanapaswa kuondoka. Waliosalia bado kuna sintofahamu hususan ikizingatiwa umuhimu wa ardhi katika kaya za eneo hilo. Je nini kinafanyika, John Kibego kutoka Uganda anatuletea makala hii.