Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Walinda amani kuenziwa leo, MONUSCO kuna ya kujifunza: Jenerali Cruz

Walinda amani kuenziwa leo, MONUSCO kuna ya kujifunza: Jenerali Cruz

Ikiwa leo ni siku ya walinda amani duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametaka nchi wanachama kutoa ushirikiano wa kifedha na askari katika vikosi vya kulinda amani akisisitiza kuwa operesheni za kulinda amani lazima zifanyike kisasa na kitekenolojia zaidi.

Amesema hayo wakati huu ambapo Umoja wa Mataifa unasema walinda amani wake wanakabiliwa na vitisho zaidi kwa kuwa wanalinda amani pasipo amani na wengi wakiuawa.

Mathalani tangu kuanza kwa ulinzi wa amani mwaka 1948 hadi sasa walinda amani 3358 wameuawa na idadi imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka.

Moja ya ujumbe wa wa ulinzi wa amani ambao ni mkubwa zaidi kuliko zote 17 duniani kote ni ile iliyoko Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, MONUSCO ambayo kamanda wake mkuu Jenerali Carlos Alberto dos Santos Cruz anasema nchi ni kubwa na changamoto ni nyingi kwa hiyo..

(Sauti ya Jenerali Santos)

“Tunahitaji kutumia mbinu mbali mbali na mikakati mbali mbali mbali kwenye maeneo tofauti hapa nchini. Pia tunahitaji kutumia mbinu zote ambazo Umoja wa Mataifa unatupatia kutekeleza majukumu yetu. Na pia nadhani hapa DR Congo Umoja wa Mataifa una fursa ya kutumia mambo mengi kujifunza.

MONUSCO ina jumla ya watendaji 20, 878 ambapo kati yao zaidi ya Elfu 19 ni askari.