Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hali ya kibinadamu ya wakimbizi wa Burundi nchini Tanzania

Hali ya kibinadamu ya wakimbizi wa Burundi nchini Tanzania

Burundi! tangazo la tarehe 27 la mahakama ya kikatiba nchini humo kumruhusu Rais Pierre Nkurunzinza kuwania kwa mara tatu nafasi ya Urais kwenye kinyang’anyiro cha uchaguzi sambamba na jaribio la mapinduzi lililofeli, vimeibua mzozo wa kisiasa na kibinadamu na maelfu ya wananchi wamekimbilia nchi jirani ikiwemo Tanzania. Hali ya kibinadamu inazorota huko kila uchao, kipindupindu kikiripotiwa, halikadhalika vifo, huku huduma za uzazi nazo mashakani. Je nini kinaendelea? Ungana na Joseph Msami kwenye makala hii.