Wakimbizi wa Kenya waliojihifadhi Uganda waanza kurejea nyumbani
Miaka saba baada ya vurugu za baada ya uchaguzi nchini Kenya zilizosababisha raia wa nchi hiyo kukimbilia nchi jirani ya Uganda hatimaye baadhi ya raia wameanza kurejea nchini mwao kwa hiari. John Kibego akiwa katika moja ya kambi za wakimbizi hao nchini humo amejihimu mapema alfajiri na kushuhudia zoezi la kuondoka kwa wakimbizi hao. Ungana naye.