Shamrashamra Liberia baada ya Ebola kudhibitiwa
Baada ya mwaka mzima wa kuishi na janga la Ebola na kusaka mbinu ya kuondokana na jinamizi hilo, hatimaye sasa Liberia iko huru kwani imetangazwa rasmi kutokuwa na maambukizi mapya ya kirusi hicho hatari. Shughuli zinarejea katika hali ya kawaida na wiki hii imeshuhudia mojawapo ya shughuli maalum ya ufunguzi wa shule ya sekondari ya kati na juu mjini Monrovia. Mamia ya watu walijitokeza katika tukio hilo kama anavyosimulia Assumpta Massoi kwenye makala hii.