Viongozi na watendaji wakuu serikalini wana wajibu kulinda misitu Afrika
Wakati kongamano la Umoja wa Mataifa kuhusu misitu, likiingia wiki ya pili jijini New York, Marekani, washiriki wa kongamano hilo wanatarajiwa kufikia makubaliano ya kimataifa kuhusu misitu. Miongoni mwa washiriki ni Godwin Kowero ambaye ni mkurugenzi shirika la misitu la African Forestry Forum lenye makao yake makuu mjini Nairobi Kenya. Kwa upande wake akiwa mwakilishi kutoka Afrika anasema kwamba bara hilo lina ujumbe mahsusi ambao unaendana na ajenda nzima ya mkutano ambapo katika mahojiano na Grace Kaneiya wa Idhaa hii anaanza kwa kueleza ujumbe huo.