Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Miradi yaleta nuru miongoni mwa jamii za wasamburu nchini Kenya

Miradi yaleta nuru miongoni mwa jamii za wasamburu nchini Kenya

Nchini Kenya jamii za wafugaji zinakabiliana na changamoto mbali mbali ikiwemo malisho ya mifugo yao wakati huu ambapo idadi ya watu na mifugo inaongezeka, na mabadiliko ya tabianchi yanaathiri upatikanaji wa mahitaji ya makundi hayo.

Mathalani miongoni mwa jamii za wasamburu, changamoto hizo ziko dhahiri lakini miradi iliyoanzishwa sasa inaleta nuru.

Jeni nini kinafanyika? Ungana na Grace Kaneiya kwenye makala hii.