Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Maelfu ya wakimbizi kutoka Yemen wanatarajiwa kuwasili Djibouti

Maelfu ya wakimbizi kutoka Yemen wanatarajiwa kuwasili Djibouti

Hali ya kibinadamu nchini Yemen inazidi kuzorota kwa kasi, na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR inatarajia kuwa katika miezi michache ijayo zaidi ya wakimbizi 30,000 kutoka Yemen watawasili pwani ya Djibouti na wengine 100,000 nchi jirani ya Somalia.

Hii ni kutokana na mzozo wa wenyewe kwa wenyewe ulioshamiri baada ya kuanza kwa mapigano baina ya vikosi vya serikali na wapiganaji wa Houthi.

Je waliokimbia Yemen na sasa wanaishi ugenini maisha yako vipi? Ungana na Joseph Msami kwenye makala hii..