Nuru yaangazia harakati za ukatili wa Kingono, DRC kuna mafanikio
Ukatili wa kingono umekuwa tishio la maendeleo na ustawi wa wanawake na watoto hususan kwenye maeneo ya vita. Vikosi vya usalama na vile vilivyojihami hudaiwa kufanya vitendo hivyo ili kujenga hofu miongoni mwa jamii bila kujali kuwa ni ukiukwaji wa haki za binadamu. Ni kwa kutambua hilo Baraza la usalama wiki hii limekuwa na mjadala wa wazi kuhusu ukatili wa kingono hususan maeneo ya mizozo ambapo maeneo ya Kaskazini mashariki mwa Nigeria yaliangaziwa. Je nini kiliwekwa bayana? Ungana na Priscilla Lecomte kwenye makala hii.