Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Elimu zaidi kuhusu asasi za kiraia na mchango wake yahitajika: Mlay

Elimu zaidi kuhusu asasi za kiraia na mchango wake yahitajika: Mlay

Vuguvugu la nafasi ya asasi za kiraia katika maendeleo hususan namna bora ya matumizi ya  rasilimali fedha linachukua kasi kimataifa amesema mmoja wa washiriki wa mkutano kuhusu uwezeshaji wa kifedha unaoendelea katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York.

Katika mahojiano maalum na Joseph Msami wa idhaa hii Bi. Jovita Mlay ambaye anawakilisha mtandao wa wanawake wa Afrika katika sera za kiuchumi, AWEPON anasema kuelekea mkutano wa ufadhili kwa ajili ya maendeleo nchini Ethiopia hamasa inahitajika zaidi. Kwanza anajibu swali nini ujumbe wa asasi anayoiwakilisha

(SAUTI MAHOJIANO)