Kumbukizi ya mauaji ya kimbari yaliyotokea Rwanda yafanyika UM
Tarehe Saba mwezi Aprili ni siku ya kumbukizi ya mauaji ya kimbari yaliyotokea Rwanda miaka 21 iliyopita. Katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa kulifanyika tukio maalum la kutafakari yaliyotokea na jinsi gani hatua zinapaswa kuchukuliwa ili kitendo kama hicho kisitokee tena, halikadhalika kuwapatia faraja wahanga wa kitendo hicho. Je nini kilijiri? Shuhuda wetu alikuwa Priscilla Lecomte..