Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mataifa ya Afrika ya Mashariki yabadilisha mawazo ya vita dhidi ya umasikini na kutokuwepo kwa usawa:

Mataifa ya Afrika ya Mashariki yabadilisha mawazo ya vita dhidi ya umasikini na kutokuwepo kwa usawa:

Wawakilishi kutoka Mataifa ya Afrika ya mashariki wanakutana Nairobi  Kenya kwenye  kongamano  maalum  ili kubadilishana  uzoefu wa   kukabiliana  na  umasikini  na  kutokuwepo  kwa  usawa .

Kongamano  hilo  la mawaziri wa maendeleo  ya jamii  limeandaliwa  na  shirika  la  Umoja  wa  Mataifa  la  elimu,  sayansi  na  utamaduni  UNESCO   ni  la  kwanza  la  aina  hiyo.

Nchi  15  kutoka ukanda wa Afrika  ya  Mashariki  wanashiriki  kata  kongamano  hilo.  Mada  maalumu  ya kongamano  hilo  ni “Haki  ya   kimataifa” ikijikita  katika  kushirikiana  uzoefu  na sera  katika  masuala  kama  kupunguza  umasikini  na  kutokuwepo  kwa  usawa.

Mjadala huo  utachangia katika maendeleo  ya ajenda  ya maendeleo  ya Umoja  wa  Mataifa  baada ya mwaka  2015.  Masuala  mengine  muhimu  wanayojadili  ni ajira kwa vijana  na maendelo  ya ujuzi, ukuaji wa idadi ya watu  na  inavyochangia katika  maendeleo  ya kijamii.

Mwisho  wa  kongamano  hilo  kunatarajiwa  mapendekezo  na kupitishwa  kwa azimio la  mawaziri  hapo  kesho Februari   26.