Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Sanaa iliyopigwa marufuku yakumbusha yaliyojiri Auschwitz-Birkenau

Sanaa iliyopigwa marufuku yakumbusha yaliyojiri Auschwitz-Birkenau

Miaka 70 iliyopita, kambi ya Auschwitz-Birkenau huko Poland iliyokuwa ni makazi ya wafungwa wenye asili ya kiyahudi ilikombolewa baada ya madhila yaliyokuwa yanatekelezwa na serikali ya kinazi ya Ujerumani.

Mengi yaliyoendelea kwenye kambi hiyo ikiwemo mateso kwa wafungwa yameendelea kufichuliwa kupitia njia mbali mbali na moja wapo ni onyesho lililoitwa Sanaa iliyopigwa marufuku.

Je ni Sanaa gani na imetumika vipi kufikisha ujumbe wa madhila yaliyokuwa yanatokea kwenye kambi hiyo?.

Ungana na Joshua Mmali kwenye makala hii.