Kampeni dhidi ya unyanyapaa na haki za wanawake na watoto
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF linasongesha harakati za mapambano dhidi ya unyanyapaa kwa waathirika wa ugonjwa wa Ukimwi pamoja na kampeni ya haki za wanawake na watoto.
Kupitia balozi wake mwema mwanamuziki Oliver Mtukudzi wa Zimbabwe, ambaye amefanya ziara maalum nchini Msumbiji na kukutana na wadau wa ukimwi na haki za makundi hayo. Ungana na Joseph Msami katika Makala ifutayo.