Hali ya haki za binadamu Bahrain inasikikitisha
Ofisi ya Haki za Binadamu Umoja wa Mataifa imeelezea wasiwasi wake kuhusu kukamatwa kwa kiongozi wa kikundi cha harakati za upinzani cha Al Wefaq, Sheikh Ali Salman, na unyanyasaji na kuweka korokoroni kwa watu wanaotekeleza haki zao za uhuru wa maoni na kujieleza. Taarifa zaidi na Joseph Msami
(TAARIFA YA MSAMI)
Katika taarifa yake , ofisi hiyo imesema taarifa za kuaminika zilizokusanywa na Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa huko Geneva, Sheikh Salman alikamatwa baada ya kuitwa kwa mahojiano katika Idara ya Upelelezi wa makosa ya jinai siku ya jumapili, siku mbili tu baada yake kuchaguliwa kwa kipindi cha nne kama Katibu Mkuu wa Al Wefaq .
Wakili wake wamesema anakabiliwa na mashtaka makubwa ambayo yanaweza kumuweka gerezani kwa kipindi kirefu ikiwa ni pamoja na wito wa kupindua serikali.
Kwa maantikia hiyo, Ofisi za Haki za Binadamu imieomba serikali ya Bahrain kumwachilia Shekh Salman na wale wote waliowekwa kizuizini kwa ajili ya kutekeleza haki yao ya msingi ya uhuru wa kujieleza na kukusanyika.