UN yaalani mashambulizi ya anga Libya
Umoja wa Mataifa umelaani vikali tukio la mashambulizi ya anga yaliyofanywa mwishoni mwa wiki katika mji wa Misrata nchini Libya na kusababisha madhara kwa raia.
Katika taarifa yake, Kamishna ya UN kwa ajili ya Libya UNSIMIL umezitaka pande zote zinazohusika katika mzozo wa Libya kujiepusha na matukio yanayoweza kulirudisha upya taifa hilo kwenye mapigano.
UN imesisitiza kuwa hatua yoyote ya kuchochea mapigano inaweza kuitumbukiza Libya katika hali mbaya zaidi na hivyo kusababisha kukosekana kwa amani ya kudumu.