Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Masahibu yanayowakumba wahamiaji

Picha: IOM

Masahibu yanayowakumba wahamiaji

Tarehe 18 Disemba kila mwaka dunia ni siku ya wahamiaji duniani. Hii ni siku mahususi kwa ajili ya kuangazia ustawi wa kundi hili ambalo kwa mujibu wa shirika la kimataifa la uhamiaji, IOM,  ni zaidi ya watu milioni mia mbili kote duniani.

Maadhimisho ya siku hii yalipitishwa rasmi na baraza kuu la Umoja wa Mataifa mnamo Disemba 4, mwaka 2000 kutokana na idadi kubwa ya wahamiaji inayoongezeka.

Hii ilitanguliwa na mkataba wa kimataifa kuhusu ulinzi wa haki za binadamu kwa wafanyakazi wote, wahamiaji na familia zao.

Basi ungana na  Asumpta Massoi katika ripoti ifuatayo.