Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wastani wa bei ya vyakula haikubadilika kwa miezi mitatu mfululizo

Bei ya vyakula yazingatia bidhaa zitokanazo na maziwa.(Picha ya FAO)

Wastani wa bei ya vyakula haikubadilika kwa miezi mitatu mfululizo

Shirika la chakula duniani FAO limetoa ripoti ya bei ya vyakula kwa mwezi Novemba inayoonyesha kwamba kwa wastani bei ya vyakula haijapanda wala kushuka kwa miezi mitatu  mfululizo tangu mwezi Septemba.

Vipimo vya bei vinazingatia mabadiliko ya bei ya vyakula ya kimataifa ikiwemo bei ya nafaka, nyama, bidha zitokanazo na maziwa, mafuta na sukari.

Ripoti ya mwezi Novemba inaonyesha kwamba bei ya mafuta na nafaka iliongezeka kidogo, huku bei ya bidhaa zitokanazo na maziwa na sukari ikishuka kidogo.

Kufuatia kusuasua kwa bei ya vyakula katika miaka ya hivi karibuni, vipimo vya bei ni vya chini ikilinganishwa na ilivyokuwa miaka minne iliyopita.

Sababu za kushuka kwa bei ni pamoja na wasiwasi kufuatia mabadiliko ya hali ya hewa.

Nchini Brazil kwa mfano, mvua iliondoa shaka ya kiangazi ambayo ingeathiri uzalishaji kwenye nchi hiyo inayoongoza kwa kuuza sukari duniani.