Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tumevuka lengo la tiba na mazishi, juhudi zinahitajika : Banbury

Harakati za kusafirisha wagonjwa wa Ebola huko Sierra Leone. (Picha:WHO/C. Black — in Sierra Leone.)

Tumevuka lengo la tiba na mazishi, juhudi zinahitajika : Banbury

Mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu na mkuu wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kushughulikia dharura ya Ebola UNMEER Athony Bunbury  amesema ujumbe huo umevuka  malengo yake ya kutoa tiba kwa asilimia 70 ya wagonjwa na kuzika asilimia hiyo hiyo kwa njia salama.

Katika mahojiano na gazeti la Newsweek la Marekani Bwana Banbury amesema lengo hilo ambalo linapaswa kufikiwa ifikapo Disemba mosi mwaka huu limevuka kwa baadhi ya maeneo lakini akaonya kuwa huenda lisitimizwe katika baadhi ya maeneo.

Mkuu huyo wa UNMEER amesema maeneo ya vijijini nchini Sierra Leone, eneo liitwalo Makeni na Port Loko ni  ya kutiiwa mkazo zaidi na kuomgeza kuwa juhudi za jumuiya ya kimataifa zinahitajika.