Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Madhara ya mabadiliko ya tabianchi kwa kilimo na biashara yajadiliwa

UN Photo/Ariane Rummery
Picha:

Madhara ya mabadiliko ya tabianchi kwa kilimo na biashara yajadiliwa

Mjadala wa uwiano kati ya mabadiliko ya tabia nchi, usalama wa chakula, kilimo na biashara  umefanyika mjini Bujumbura Burundi ukiwaleta pamoja  wataalamu wa sekta hizo kutoka nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), wanadiplomasia na watunga sera.

Mjadala umefanyika ikiwa ni takribani mwezi mmoja na Nusu baada ya kikao cha baraza kuu la Umoja wa Mataifa ambacho kiliangazia mabadiliko ya tabia nchi duniani , ikiwamo mipango na malengo ya kunusuru sayari dunia katika madhara yatokanayo nayo. Washiriki wameangazia jinsi ya kuweka sera zenye uwiano kwa sekta tajwa. Mathalani utekelezaji wa lengo namba Moja la maendeleo ya milenia la kupunguza umaskini ambalo lapaswa lisiathiri mazingira.

Halikadhalika hoja ya viwanda visivyoathiri mazingira isiathiri usalama wa chakula au uzalishaji viwandani.

Lakini nini ilikuwa  maazimio ya ya mkutano huo? Na zaidi walengwa yaani wakulima na wale wanaofanya shughuli zinazohatarisha mazingira wana mtazamo gani? Mwandishi wetu wa maziwa makuu Ramadhani Kibuga amevinjari mkutanoni na kwa wananchi na kituandalia taarifa ifuatayo.