Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ukatili wa makundi yaliyojihami kwa misingi ya kikabila na kidini ni changamoto: Kamishna Zeid

UN Photo/Paulo Filgueiras
Kaminshna Mkuu wa haki za binadamu kwenye Umoja wa Mataifa Mwanamfalme Zeid Ra’ad Hussen. Picha:

Ukatili wa makundi yaliyojihami kwa misingi ya kikabila na kidini ni changamoto: Kamishna Zeid

Kamishana wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Zeid Ra’ad Al Husssein amesema wakati wa ufunguzi wa maadhimisho ya miaka thelathini ya kupitishwa kwa Mkataba dhidi ya Mateso na Ukatili kwamba, mkataba huo ni chombo muhimu cha sheria ya kimataifa, lakini licha ya maendeleo ya kila siku, katika kila bara, wanawake, wanaume na watoto wanateswa kwa makusudi na mawakala wa serikali.

Katika taarifa, Kamishna Mkuu Zeid amesisitiza changamoto za kuendelea kuutekeleza mkataba huo, zikiwa ni pamoja na matumizi ya nguvu kupita kiasi na ukatili dhidi ya makundi ya kikabila na kidini unaotekelezwa na makundi yaliyojihami yasiyokuwa ya kiserikali na hali mbaya mno ya haki za binadamu za wahamiaji.

Katika ujumbe wake, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon amesema kuwa mateso yanayoendelea kote duniani yanaathiri pakubwa watu binafsi na jamii, akisisitiza jukumu muhimu la mashirika yasiyokuwa ya kiserikali na ya kiraia katika kutimiza malengo ya mkataba dhidi ya mateso.

Aidha, Ban amesema, nchi zinapaswa kuchukua hatua mathubuti za kutokomeza mateso na kurejesha waathirika katika hali yao ya awali.