Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tanzania, Kenya, na Uganda zang’ara kiteknolojia

Picha: FAO

Tanzania, Kenya, na Uganda zang’ara kiteknolojia

Wakati mkutano kuhusu mipango thabiti ihusuyo teknolojia ukiendelea nchini Korea Kusini Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO, shirika la wanawake UN Women  ni miongoni mwa taasisi zilizopewa tuzo za kutambua mchango wa kuendeleza maisha ya wanawake kupitia teknolojia.

Mkutano huo unaoratibiwa na Shirika la kimataifa la mawasiliano ITU pia umeshuhudia nchi za Afrika kama Nigeria zikipata tuzo lakini kubwa zaidi zile za Afrika Mashariki zimeandika historia kwa kuingia   katika baraza la utawala la ITU kwa mara ya kwanza.

Katika mahojiano na idhaa hii kutoka Korea Kusini mkuu wa mawsiliano wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA Innocent Mungi anadadavua vyema siri ya mafanikio hayo hususani ni kwa nchi yake na pia kueleza mambo mengine muhimu yanayojadiliwa katika mkutano huo. Kwanza anaanza kwa kueleza kuhusu utolewaji wa tuzo.

(SAUTI MAHOJIANO)