Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mafuriko yaathiri maisha ya wakimbizi Kenya

Leonie akiwa nje ya makazi yake na wanawe wanne. Ni mjane baada ya mume wake kufariki kufuatia mafuriko ambayo yaliwafurusha wengi kutoa kambi ya Kakuma nchini Kenya.(Picha ya UNHCR/C.Wachiaya)

Mafuriko yaathiri maisha ya wakimbizi Kenya

Shirika la Umoja wa Mataifa la wakimbizi UNHCR nchini Kenya linafanya kila liwezekanalo kunusuru maisha ya wakimbizi kutokana na mafuriko katika kambi za Kakuma na Daadab nchini humo.

Afisa wa UNHCR nchini humo Emanuel Nyabera ameiambia idhaa hii kuwa mafuriko hayo yamesababisha kifo cha mtu mmoja katika kambi ya Kakuma na kwakuwa amsimu wa mvua unaendela UNHCR inahakikisha usalama wa wakimbizi katika kambi hizo ikiwa ni pamoja na kudhibiti magonjwa ya milipuko yatokanayo na mafuriko.

(SAUTI NYABERA)

Akizungumzia hatua zinazochukuliwa na UNHCR katika kujihami dhidi ya mafuriko nchini Burundi mwakilishi mkazi wa UNHCR nchini humo Abel Mbilinyi anasema

(SAUTI MBILINYI)