Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wanaojidai ni wanamgambo wa kiislamu wanapotosha uislamu: Mjadala

Sheikh Abdullah Bin Bayyah (Kulia), Rais wa jukwaa la kuendelea amani miongoni mwa jamii za kiislamu akiwa na Waziri wa masuala ya dini kutoka Mali Anadou Diallo (kushoto) wakati wakizungumza na waandishi wa habari baada ya kikao cha ngazi ya juu kilichojadili masuala ya ugaidi. (Picha: UN /Amanda Voisard)

Wanaojidai ni wanamgambo wa kiislamu wanapotosha uislamu: Mjadala

Tarehe 30 Septemba mwaka 2014 katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa kulifanyika kikao cha kamati ya Baraza la Usalama la Umoja huo kinachohusika na harakati za kutokomeza ugaidi.

Kikao hicho kilichoandaliwa kwa pamoja na kamati hiyo na Morocco, kililenga kupata uzoefu wa nchi hiyo ya kifalme katika kukabiliana na ugaidi. Mali na Guinea ambazo zimetajwa kunufaika na mfumo wa Morocco nazo zilizoa ushuhuda wao huku washiriki wakiangazia kile kilichoibuka cha baadhi ya vikundi vilivyojihami kujiita kuwa ni vikundi vya kiislamu.

Je ni yapi yalijiri? Basi kwa kupata muhtasari wake, ungana na Assumpta Massoi kwenye makala hii.