Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ban akaribisha ubadilishanaji mamlaka kutoka MISCA kuwa MINUSCA huko CAR

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati MINUSCA yazinduliwa rasmi na rais wa nchi hiyo Catherine Samb-Panza na Herve Ladsous, Mkuu wa operesheni za ulinzi wa amani wa Umoja wa Mataifa.

Ban akaribisha ubadilishanaji mamlaka kutoka MISCA kuwa MINUSCA huko CAR

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amekaribisha kuanza kwa mamlaka mpya ya ulinzi ya Umoja huo ya kulinda amani huko Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, MINUSCA kutoka ile ya awali ya Muungano wa Afrika, MISCA.

Kubadilishana huko kwa mamlaka kumefanyika baada ya kukamilika  kwa muda wa MISCA na hivyo kuashiria  mwanzo wa hatua ya kijeshi na polisi ya MINUSCA huko CAR.

MINUSCA ina wanajeshi 6500, polisi 1000 na kundi la watendaji wa kiraia na wanaendelea kusambazwa maeneo mbali mbali ya nchi hiyo na lengo kuu ni kuimarisha ulinzi na usalama wa raia na kusaidia mchakato wa kisiasa na ujenzi wa nchi.

Katibu Mkuu ameshukuru MISCA na vikosi vya Ufaransa  kwa kulinda maisha ya watu wengi.

Halikadhalika ameshukuru  ushirikiano kati ya  Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika pamoja na kuhakikisha makabidhiano muafaka wa mamalaka, kwa mujibu wa viwango Umoja wa Mataifa.