Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baraza la Usalama lalani mauaji ya Haines

Baraza la Usalama.Picha ya UM

Baraza la Usalama lalani mauaji ya Haines

Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limelaani vikali mauaji ya

mfanyakazi wa misaada ya kibinaadamu wa Uingereza Bw David Haines,

yaliyofanywa na kundi la ISIS.

Bwana Haines ni mateka wa tatu mgeni kuchinjwa na kundi la ISIS, kundi

ambalo katika miezi ya karibuni limetanua udhibiti wake nchini Syria

na kaskazini mwa Iraq.

Wajumbe hao wa nchi 15 pia wametoa rambirambi kwa familia ya marehemu,

serikali ya Uingereza, pamoja na familia za watu wote walioathiriwa na

kundi la ISIS.

Pia baraza hilo limesisitiza haja ya kukusanya nguvu ya pamoja ili

kuvishinda vitendo hiovu vinavyofanywa na kundi hilo linalotishia

kuanzisha Dola ya Kiislamu. Juzi usiku kundi la ISIS lilitoa video

inayoonesha Haines akichinjwa.