Mchezaji soka Drogba ni mshirika vita dhidi ya malaria
Lengo namba sita la malengo ya maendeleo ya milenia ni kupambana na ukimwi, malaria na magonjwa mengine. Katika kampeni yake ya kutokomeza malaria duniani, Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendelo UNDP limeshirikisha balozi wema wake, mchezaji wa mpira Didier Drogba, katika video fupi ambapo anapigana na mbu. Angalia video hii na usikose kusikiliza makala ya Joseph Msami!