Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Harakati za kukabiliana na Ebola zaendelea

Uwanja wa ndege wa Lugin nchni Sierra Leone, mtaalamu wa afya kutoka WHO akipima joto la abiria ikiwa ni harakati za kudhibiti Ebola. (Picha:WHO-Sierra Leone)

Harakati za kukabiliana na Ebola zaendelea

Ebola! Ebola! Ebola! Ugonjwa uliotikisa eneo la Afrika Magharibi kuanzia mwezi Machi mwaka huu ukijikita katika nchi Guinea, Liberia, Sierra Leone na hivi karibuni Nigeria. Hadi sasa watu zaidi ya 1500 wamefariki dunia kutokana na ugonjwa huo. Shirika la Afya duniani kwa kuona dharura itokanayo na ugonjwa huo ilichukua uamuzi wa haraka wa kuruhusu matumizi ya dawa ambayo bado haijafanyiwa majaribio ili itumike kutibu wagonjwa wa Ebola. Hiyo ilikuwa ni moja tu ya hatua zilizochukuliwa kando ya nyingine nyingi. Je ni zipi hizo? Na wananchi wanachukulia vipi hatua hiyo? Basi ungana na Joseph Msami kwenye makala hii kuhusu Ebola!