Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM wasikitishwa na tetemeko la ardhi China

UN Photo/Mark Garten)
Katibu Mkuu Ban Ki-moon. Picha:

UM wasikitishwa na tetemeko la ardhi China

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon ameeleza kusikitishwa kwake na vifo vya watu na kuharibika kwa majengo na miundombinu katika maeneo ya China kusini, kufuatia tetemeko la ardhi lililotokea jimbo la Yunnan, siku ya jumapili.

Taarifa ya msemaji wake imemkariri Ban akituma rambirambi kwa serikali ya China na familia za wahanga huku akiwapa pole majeruhi na wote walioathirika na tetemeko hilo.

Amesema Umoja wa Mataifa uko tayari kutuma msaada wake ili kukidhi mahitaji ya kibinadamu na kuratibu misaada ya kimataifa.