Mkaguzi wa Serikali ya Tanzania akagua Umoja wa Mataifa
Wakati ripoti ya Ukaguzi ya Umoja wa Mataifa kwa mwaka 2013, ikitolewa rasmi leo tarehe 24, Julai, idhaa ya kiswahili imepata fursa ya kuongea na Bwana Ludovic Utouh, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye pia ameteuliwa rasmi na Baraza Kuu kuwa mwanachama wa Bodi ya Ukaguzi wa Umoja wa Mataifa, mwaka 2012.
Ana mtazamo gani kuhusu shughuli za ukaguzi kwa ngazi ya kitaifa na ya kimataifa? Basi ungana na Priscilla Lecomte kwenye makala hii.