Ban Ziarani Haiti
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon, ambaye yupo ziaraniHaiti, leo anatarajiwa kukutana na timu ya Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo, MINUSTAH.
Hii leo pia Bwana Ban anatarajiwa kuzindua rasmi kituo cha michezo kiitwacho “Michezo kwa Tumaini”nchini humo, akishirikiana na rais wa Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki (IOC) Thomas Bacth.
Hapo jana Bwana Ban alikutana na kufanya mazungumzo na rais nchi hiyo.