Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mwakilishi wa UM Somalia alaani mauaji ya mbunge "Hayd"

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu na Mkuu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa nchini Somalia, UNSOM, Nicholas Kay

Mwakilishi wa UM Somalia alaani mauaji ya mbunge "Hayd"

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia, Nicholas Kay, amelaani vikali mauaji ya mbunge Mohamed Mohamud “Hayd” na mlinzi wake yaliyotokea leo asubuhi mjini Mogadishu, akieleza kutiwa wasiwasi na mashambulizi kadhaa yanayodaiwa na kundi la Al-Shabab tangu mwanzo mwa Ramadan.

Nicholas Kay amesema, mwezi wa Ramadan ni mwezi wa amani na maridhiano, na kuuawa watu wakati wa mwezi huu ni dalili ya kuwa watekelezaji hawa hawajali maisha ya Wasomali.

Mwakilishi huyu ameiomba serikali ya Somalia iwapeleke waliotenda mauaji hayo mbele ya sheria haraka iwezekanavyo, akisisitiza msimamo wa Umoja wa Mataifa kuziunga mkono juhudi za wananchi na wawakilishi wa Somalia ili kuleta amani ya kudumu nchini.

Hatimaye, amepeleka rambirambi zake kwa familia za wahanga na Bunge la Somalia.