Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Umoja wa Mataifa waingia na wasiwasi kuhusu vurugu za Libya

UN Photo/Iason Foounten
@

Umoja wa Mataifa waingia na wasiwasi kuhusu vurugu za Libya

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa usaidizi nchini kwa ajili ya kuipiga jeki Libya

imesema kuwa inaendelea kufuatilia kwa karibu yale yanayoendelea

kujitokeza katika taifa hilo hasa katika eneo la Benghazi. Taarifa zaidi na George Njogopa.

Katika taarifa yake UNSIMIL imelaani vikali mauwaji yanayoendelea

kwenye eneo hilo na kutoa wito kwa pande zinazozozana kujiepusha na

vurugu.

Kumekuwa na mlolongo wa mapigano baina ya makundi yanayohasimiana na

kusabisha watu kadhaa wamepoteza maisha huku wengine wakijeruhiwa.

Hali ya waiswasi imeendelea kulikumba eneo hili na hakuna dalili ya

kupatikana suluhi kutokana na kuongezeka kwa matukio yanayoambatana na ugaidi

Ujumbe huo wa Umoja wa Mataifa umezitaka mamlaka za kidola

kuchukua hatua za haraka kudhibiti hali hiyo korofi ambayo inazidisha

kitisho kwa maisha ya raia.