Afya ya uzazi ni moja ya suala linalopswa kushughulikiwa miongoni mwa jamii za watu wa asili
Suala la afya ya uzazi hususan kwa wanawake wa jamii za asili ni jambo linalokumbwa na changamoto nyingi kwa sababu ya mila potofu ikiwemo ukeketaji haswa. Mila hiyo yatekelezwa na jamii ya waSamburu nchini Kenya ambapo Justine Lesiano anayeshiriki kikao cha kudumu kuhusu watu wa asili hapa New York ameieleza idhaa hii kuwa ni jambo analoeleza kwenye kikao hicho.
(Sauti ya Lesiano-1)
Bi Lesiano ambaye anatoka shirika la Illaramata linaloelimisha wanawake na jamii kuhusu maswala mbali mbali ametoa shukrani zake kwa Umoja wa Mataifa kwa mafunzo ambayo wameyapata na ambayo yatanufaisha jamii.
(Sauti ya Lesiano 2)