Wanawake watendewe haki zao katika jamii za watu wa asili
Wakati kikao cha kudumu kinachohusu haki za watu wa asili kikiingia siku yake ya pili hii leo hapa mjini New York, wawakilishi wameangazia hali ya afya ya wanawake katika jamii hizo, ambayo kwa takwimu zilizoonyeshwa, ni tete zaidi.
Martha Ntoipo mwakilishi wa wanawake wa kimasai kutoka Tanzania ameiambia Idhaa hii umuhimu wa kuendelea kutetea haki za wanawake kwa watu wa asili.
(Martha-1)
Aidha, amezungumzia maudhui ya mwaka huu ya kikao hicho, ambayo ni utawala bora, kwa kuzingatia umuhimu wa ushirikiano wa wanawake katika siasa kwa ngazi ya kitaifa.
(Martha-2 )
Hata hivyo Martha anasema hamasisho analotoa kwa jamii na wanawake wa kimasai imeleta mafanikio…
(Martha-3 )